Jumanne, 6 Septemba 2016

TAMU NA CHUNGU

sehemu ya tatu



Yahaya; Ndugu yangu najua wajua fika kuwa wiki kadhaa tu koo yangu ilipatwa na tatizo na kuondokewa na mmoja wa ndugu muhimu sana ndio nalijua hilo si kuhusu kufariki kwa Bwana Matango {kudu alidakia} haswa sasa na ndhani wakumbuka kuwa adhima yangu ni kuwa na mimliki kubwa na nzuri na pahala pa kufanikisha hili ni katika kushika milki ya huyu ndugu yangu na swala hili litatukia baada ya wiki ya pili ya msiba kwisha yaani siku ya kuanua matanga wote tutakapokuwa  kwenye kikao cha wazee wa koo shida ni kwamba taratibu za koo hazinipi ruhusa ya kushika mali hizi rafiki yangu naomba busara zako kwani kichwa changu kina chemka.
Kudu;mhh sasa hapo mie sidhani kama nitakuwa na uwezo wakufanza lolote maana kuna mambo ambayo unataka kuchanganya na mwisho wake uwaga sio mzuri  kakangu
Yahaya; kwanini ushindwe na mambo gani hayo  unayoyaongelea wewe?


Kudu;Unajua vitu tunavyofanya sikuzote uwa ni mabaya ila kwakuwa tunafanya kwa maslai binafsi uwa tunafanya kuwa halali ila katika swala hili na maelezo yako hayo hapo kuna busara za wazee na tambua fika maamuzi yao uwa hayapingwi kwakuwa wanatumia hekima zao pili kuna mila na desturi katika jambo hili hata kama nitakupa mashauri ukumbuke hii miiko iliyopo kwenye jamii yetu haswa katika jambo hili ulilokujanalo.
Yahaya;Sawa hayo yote nayatambua vyema lakini namie nina matamanio yangu na ndio sababu ya kukutafuta na kukuleta mpaka pahali hapa nakutambua vyema bwanaKudu na nina imani kuwa hata wewe wanitambua vilivyo na hali zangu wazijua  fika sina hakika kuwa utaniona lofa au kuniweka katika kundi la wapuuzi kwa maamuzi haya niliyonayo
Kudu;kwasasa saivi ndo naelewa adhima yako vilivyo na naomba ukumbuke mambo mawili yale niliyosema ukisha kubaliana nayo hapo nami nitakuwa na nafasi ya kueleza maono yangu ili tusiweze kulumbana sana nakubaliana nayo {ilikuwa sauti ya kinyonge toka kwa Yahaya} hapo sawa sasa jambo la kwanza ilikuweza kushawishi hisia na busara za wazee pamoja na mamaChiku mwenyewe badili msimamo wako uwe chanya kwa watu wote hawa
kohkohhkohoKudu alitoa kikohozi cha kusafisha koo lake iliaweze kusikika vyema kisha akaendelea kama utafanya shingo yako kuwa ngumu katika hili tambua fika mawazo ya wazee yatakuwa kinyume na wewe na tena katika mila na desturi za hapa linapotokea swala kama hili wazee wanaangalia hali ya familia husika na kama mama wa familia anajiweza wao umpatia jukumu la kutafuta mtu wa kumrithi na kummilikisha mali zote binafsi yangu naona hii ni nafasi pekee ya kumshawishi mamachiku kukubaliana na matakwa japo sio kwaku mueleza yale utakayo laa ila jaribu kuteka ule ukaribu wako kwake sijui kama tu pamoja.
Yahaya;mmmh mh haya maji ya shingo ila hakuna tatizo ngoja nitaona itakavyokuwa kabla ya siku kufika
Maono ya yahaya sasa yalikuwa yakiwaza utajili wa mali kedekede na kupewa mtu wa kupokea kauli na maagizo yake bila kuhoji nini cha ziada moyoni mwake hakuwa na lepe la huruma kwa familia hii iliyojawa majonzi
Kudu;ndugu yangu swala lolote linanalo hitaji mikono na busara za wazee uwa sio jambo jepesi lakini nadhani itafaa kama ukimrithi na mfiwa mwenyewe
Yahaya;mmh eeenh hapo hapa tena ilo swala hata silitaki kabisaa…yani pale mie nataka mali tu maisha ya chiku na mamaye sitaki yawe yangu hata punje.
Kudu;basi hapo ndo unapokosea ila hakuna namna na mie mpaka sasa sina la kuongeza kama kila neno unaona mzigo hapo namie na nanawa mikono kaka tusubiri maamuzi ya balaza la wazee hatuna uwezo wa kuingilia watakachotaka kufanya.
Yahaya;mwee sawa rafiki yangu katika hili nimeingia mkenge ila katika ukoo wote mie ndo mkubwa na hili swala hakika litakuja kwangu tu.
Kudu;sawa tusubiri ….. af wakati unatuacha ebu tuanze kurejea
Wakati haukuwa rafiki kwao ilibidi wanyanyuke nakuanza kujerea majengo Yahaya hakuamini kama swala hili limekuwa gumu kiasi kwamba hata kudu alikuwa na nafsi ya uwoga kutoa na kueleza mashauri yake juu ya namna ya kulifanikisha na njia nzima bado alikuwa akiona giza kubwa kwani hakuona hatma ya kile alichokuwa akitaka kupata.

Akiwa katika chumba chake Kapemba bado alikuwa na taswira nzito kwa kujaribu kutengeneza picha ya namna ambavyo kijana wa umri wake anavyokutana na changamoto nzito na kukosa msaada wa kuzitatua,alijaribu kufikiria hali ya maisha katika kijiji chao ilivyokuwa hapo awali na kulinganisha na hali aliyoipata katika sauti ya Sada katika siku ile marazote alipotaka kupata usingizi sauti na sura ya huzuni iliyokata tamaa ya rafikiye kipenzi sada ilijitokeza na kufanya usingizi kuwa wenye maruweruwe mengi hapana nitasema na Baba kesho labda atakuwa anajua chanzo {alijisemea Kapemba na kulazimisha kujilaza}


Usikose kufuatiali sehemu ijayo..............