ILIPOISHIA
Siku Zote nilijibidisha kuwa mfano bora ili niweze kupata mchumba, nilikuwa mtiifu, nikiwa heshimu wenzangu na kushirikiana nao vema kujenga Taifa.Kujaribu kuwa na marafiki wengi wa jinsia tofauti.
ENDELEA
Nilijitahidi nikihisi pengine wale marafiki wangenifaa kumbahatisha wa ubani wangu.
Pamoja na yote hayo sikuweza kubahatika kupata niliyempenda kutoka moyoni, na aliye ni penda, Nilizidi kumuomba Mungu anishushie neema ya kumpata wa ubani wangu.
Ikafikia wakati nikaomba ushauri, lakini wale niliowaomba
ushauri walionekana kuwa fukara wa mawazo, Walinishauri wakisema kuoa ni
kuoa.Eti mwanamke ningemfunza mimi mwenyewe kama atakuwa na tabia
mbaya.
Nikafikiri mara mia mia ushauri wao nikaona haukuwa na maana zaidi ya upofu.“Bw #kagoma inamaana uwingi wa wanawake ulimwenguni umekosa umpendaye?” Lilikuwa swali nililoulizwa na rafiki yangu katalambuga .Hatahivyo nilishndwa kumjibu na hatimaye nikamdharau.“Inamaana kuchagua mke wa kuishinae ni
kosa????, pengine ni kama kupewa mtihani wa somo usilo jua na kusubiri
matokeo mazuri??? au hili swala ni sawa na kuokota fungu la samaki
sokoni ama vipi?”Nilijiuliza Maswali mengi bila kujijibu kwa wakati huo.
Itaendelea tena

