sehemu ya pili
Kwao hakina chiku bado kulikuwa na songombingo la
yahaya kutaka maamuzi ya wazee wa kaya ya mmpendekeze yeye kama ndiye mtu
astahiliye kupewa mirathi japo kwa mujibu wa taratibu yahaya hakuwa mtu sahihhi
anae faha kupewa miliki na mali za babake chiku alitambua fika kuwa kwa njia za
kawaida hatoweza kuwashawishi wazee wale kukubaliana na mawazo yake pale
itakapo wadia siku ya kuanua matanga,ikiwa ni jioni tulivu yenye upepo mwanana
huku mida ikiwa inazidi yoyoma kuutafuta kigiza cha usiku aliona bora aende
kilingeni kumtafuta rafikiye Kudu mawazoni mwake aliweka imani kuwa kutoka kwa
rafiki yake huyu hatapata mawazo safi ya kufanya aweze kufanikisha mipango yake
ya kupora na kumiliki mali za
MzeeMatango nyakati zote hawapo katika shuruba kudu ndiye aliyekuwa kimbilio
lake na nyakati zote uwa asitikusilikiza mashauri anayopewa na rafikiye huyu moyoni
mwake yahaya hakuwa hata na chembe ya huruma kwa hali watakayo kuwanayo wakina
chiku pamoja na mamaye alichojali yeye ni kupewa miliki na kuzitumia mali hizi
kwa namna itakayo konga nafsi yake vilivyo aliwaza anasa kuliko maisha ya
upweke yatakayo anza kwa mama chiku na bintiye.
baada ya kufika kilingine alianza kupepesa macho kutafuta pahala alipoketi kudu
ilichukua kama dakika mbili
tu taswira ya kudu ilikuwa tayari katika mboni za macho yake mazoea ya kuwa
wote kilingine yalimfanya yahaya asipate tabu sana kuzungusha mijicho yake ili
kumpata rafikiye maana kudu alipendelea kukaa katika kona ya kati kalibu kabisa
na kitijoto cha mamamuuza.
Nyakati
zilikuwa zimesonga tangu alipoanza mwendo kwenda kilingeni jioni sasa nayo
iliyoyoma na nuru ya jua ilianza kupoteza mwanagaza wake sababu ya usiri mzito
wa mambo waliyotaka kuzungumza yahaya hakuona kama itakuwa busara kwa wao
kuketi na kuendesha mazungumzo yao katika kilinge ila hakuwa na nguvu ya
ushawishi kumuondosha kudu katika mazingira yale.
Yahaya; Habari ndugu yangu ,,,? Naona upo hapa
kupumzisha akili kama ilivyo ada.
Kudu; aaahnahaha yahaya kijogoo cha mji mtu mwenye
adhi yake ,, karibia sana kakamkubwa hapa si tupo tunaondoa mikosi na laana za
wazee wa ardhi hii ya imarakaseko.
Yahaya; nakuona tu hapa maana upo na mashamshamu leo
vipi mbona wale warembo wa pembeni hawapo pamoja nawe kunani? Umeanza yale mambo ya ajabu nisiyopenda
(Kudu alilalama) basi tuachane na haya ndugu yangu mguu huu niwako nimekuja
kukungata sikio ilikupata busara zako yahaya
alisita kidogo
Kudu; endelea nakusikiliza mbona upo kimya tena ….!
kama ni jambo la usiri sana tufanye kuzungumza baadae tukitoka hapa au we wasemaje ?
Yahaya; rafiki yangu kama nilivyosema huu mguu ni wako
na hapa sikuja kwa adhima nyingine yoyote ile zaidi ya kutaka kuonana nawe
kuzungumza jambo hili basi,maana ili jambo lina ninyima raha na Amani ya
kufanya mambo mengine hata kama nitajilazimisha vipi bado nakuwa sina uhuru
kama awali napolifikiria swala hili sasa naomba tutoke hapa twende nje kidogo
naitaji busara zako, mmmh kweli ili jambo
la hatati sana mtu mzima mwenzangu mpaka umekuwa na hali ama kweli muungwana
akivuliwa nguo sharti achutame haya twende huku njee {kudu alikubaliana na
mawazo ya yahaya kisha wote wakanyanyuka na kuanza kwenda nje ya kilinge}
Kudu; haya mkubwa mwenzangu ebu ni habarishe kuhusu
ilo swala maana ushaanza kutia ofu namie hapa naona nafsi inajawa mashaka Je kunani
huku au lile sekeseke la wale wafugaji kutoka katika ardhi ya udongo mzuri
limekuja tena?
Yahaya; hapana sio jambo hili walasindani kama lile
swala la weza kurudi tena hili la leo ni jipya tena jipya haswa, skiliza ebu
twende hapo kwenye mawe ya mtemi tukaketi hatuwezi kuongelea hili jambo hapa
rafiki yangu
Kudu
hakuwa na kinyonge wala hakutaka kubishabisha sana juu ya maombi ya yahaya
japokuwa alitambua fika kuwa tayari raha zake zimekwisha katishwa na hatapata
nafasi tena ya kuzirudia kwa wakati ule maana tayari nyakati zake zilikuwa
zimekwisha muacha alifuatana na rafikiye mpaka katika sehemu ya mawe ya mtemi
Kudu; bwanamkubwa haya sasa tumefika ebu keti na
unihabarishe juu ya hayo maswala yako nakuona hauko sawa na nadhani hata moyo
wako pia una shuruba sawa na hali ya macho yako nipo hapa sema nami
Yahaya; Ndugu yangu najua wajua fika kuwa wiki kadhaa
tu koo yangu ilipatwa na tatizo na kuondokewa na mmoja wa ndugu muhimu sana ndio nalijua hilo si kuhusu kufariki kwa
Bwana Matango {kudu alidakia} haswa
sasa na ndhani wakumbuka kuwa adhima yangu ni kuwa na mimliki kubwa na nzuri na
pahala pa kufanikisha hili ni katika kushika milki ya huyu ndugu yangu na swala
hili litatukia baada ya wiki ya pili ya msiba kwisha yaani siku ya kuanua
matanga wote tutakapokuwa kwenye kikao
cha wazee wa koo shida ni kwamba taratibu za koo hazinipi ruhusa ya kushika
mali hizi rafiki yangu naomba busara zako kwani kichwa change kina chemka.
Kudu;mhh sasa hapo mie sidhani kama nitakuwa na uwezo
wakufanza lolote maana kuna mambo ambayo unataka kuchanganya na mwisho wake
uwaga sio mzuri kakangu
Yahaya; kwanini ushindwe na mambo gani hayo unayoyaongelea wewe?
Usikose kufuatilia sehemu ijayo.
