Jumatatu, 7 Desemba 2015

SAFARI YA ISOKE

Hapo ndo nilipokuwa na CHOCHEA hasira zao zaidi mpaka Ulifika wakati baba na mama walitaka kuniachia laana na hapo ndo nika kumbuka pia maneno ya sharon na angnes baada ya kuwadanganya wazazi wangu zaidi ya miaka kumi toka nipate pesa na kuwajengea nyumba.


Japo maneno ya kina agnes na sharon  yalikuwa magumu kueleweka kwangu kulikuwa  na msingi kidogo kwa waliyosema na hawa ndo kidogo nilikuwa naona kama wananiwazia mema ila sio kwa 100% sababu wote hawa walikuwa wanakaa kwenye vikao vya kunisema pale ofisini Agnes alinambia kaka maisha ni safari ndefu ila usikate tamaa mie pia nilipitia uko uko kwan wazazi wangu walikataa mtu niliye mpenda kwa dhati na nilikuwa tayar kumvumilia kwa kila hali
lakini......chokochoko za ndugu zake na maisha waliyoleta hapo ilikuwa bala Sauti ya sharon pia ikanijia boss wangu Pole ila haya ni mapito tu ujakosea sana maana sisi wanawake tuna vimbwanga vingi sana leo utaniona nmetulia kesho ukinipa nachotaka tu tena kwenye kiapo ndoa wewe tena basi si unaona kila siku watu wanavyo lia umo majumbani ILA ANGALIA UZEE UO UNAKUJA kakangu.

Nilizid kukosa amani zaid ya ilivyokuwa awali maana maneno ya #Mzee yalikuwa tishio zaid
Na kilicho kuwa kina ni vuruga kabisaaaaaaaaaaaaa na kunitoa katika mstari wa AMANI ni icho kisa cha jamaa yangu kadinko Baada ya kupata kizunguzungu kwa kufikiria nini itakuwa hatma ya hili swala langu mawazo yali rudi upya tena kwenye mkasa wa kadinko ambao huu pekee ndo ulikuwa tishio katika swala langu la kutafuta, kupata na kukuamini #mwanamke yoyote kuwa mke wangu
Nakumbuka siku izo nili toka tu katika shughuli za ofisini na kwa bahati nzuri nilikutana na evad kwa utani tu nikamuliza ivi hayo una andika yamekupata wewe nini? Au kuna ndugu yako yasha mkutaaa?? akanambia hapana bhna haya maisha tu yana mambo mengi na hayo ndo ya nafanya akili iende mbali ivo DAH ila kweli sasa acha mie niende kwa jamaa angu Kandiko

Jumatano, 11 Novemba 2015

SAFARI YA ISOKE

Watu wengi walio ni ona walinishangaa sana, kwani sikuwahi kuonekana na mwanamke yoyote katika ukarbu ule wa kuhisiwa kuwa nina #uhusiano au niliyeongozana naye katika maisha yangu nakumwita mchumba . Si kwamba nilikuwa na hitilafu yoyote mwilini japo mawazo ya wengne hasa wasichana na wanawake niliokuwa nafanya nao kazi pale ofisini yalinipa ofu baada ya kumsikia  msaidizi wangu wa kike(secretary) alipokuwa anateta na wenzake kuwa #jogooWanguHapandiMtungi kwa kipindi chote cha kazi sikuwahi kumuonyesha ishara yoyote ya kumtaka na kilicho ni kera zaid ni kusikia toka kwa wanaume waliokuwa chini yangu kuwa #mtotomimiSirdhki na wazazi wangu wamepata hasara.Hapana nilikuwa mwanaume rijali, na sikupenda kujihusisha na ngono,kwani magonjwa yamezagaa kama inzi kwenye mzoga.


Licha ya magonjwa, ni dhambi kubwa kuzini nje ya ndoa. Nilitambua kwamba jambo hilo halimfurahishi muumba hata kidogo.Siku zote nilikuwa nikijilaumu,ikafikia wakati nikitaka kuokota mwanamke hata baa,lakini nika kumbuka kisa cha jamaa mmoja anaitwa kadinko ila ye anapenda kujiita kado wakat yeye anatafuta mtu wa kuishi nae alipata tabu na kupitia kipind kigumu kama mimi, ila yeye alikuwa na haraka kidogo hali iliyo fanya akagombana mpaka na dadake violeth miez mitatu kabla ya ndoa  kufika na kwan dadake akukubaliana na swala la kuolewa kwa uyo bint ambae bwana Kandiko ali mchagua na kuona kuwa anafaa kwani hakutaka kabisa kusubr kwa kipind chote bila kuwa na uyo bint kama mwenzi wake.


kwani imani yake ili kuwa na msukumo kuwa tabia za wana ndoa ujengeka nakuwa safi baada ya kuwa pamoja akasahau kabisa sio tu maneno aliyo ambiwa na dadake bali ali sahau hata maneno ya #wahenga kuwa #MkemwenyetabianjemaniNgaokwamumewe Aliyakumbuka maneno haya baada ya mambo yake kumwendea mlama wiki moja kabla ya  #shereheyaHARUSI yake kufanyika Kilinitisha Sana kisa cha kuvunjika kwa harusi ya kadinko kabla hata sijaweka wazi juu ya mkasa uo kuna kosa ambalo wazazi wengi wana fanya na kwao uona ni vyema tu, Yaani binafsi yangu Nilihitaji kuwa na subira nikihisi pengine ningempata atakaye nipenda na mimi kupenda.

Umri wangu ulisogea kufikia miaka arobaini. Hali ambayo iliwaogopesha sana wazazi wangu,waliokuwa wazee wa kujikongoja.  Nilizaliwa mtoto pekee wa kiume na dada zangu watatu.Wazazi wangu walichoka na maneno yangu.“Bado umri wa kuona. Nitaoa Mungu akipenda,mke mwema hupewa na Mungu” Miaka yote huwa nilikuwa najitetea hivyo .
Hapo ndo nilipokuwa na CHOCHEA hasira zao zaidi mpaka Ulifika wakati baba na mama walitaka kuniachia laana na hapo ndo nika kumbuka pia maneno ya sharon na angnes baada ya kuwadanganya wazazi wangu zaidi ya miaka kumi toka nipate pesa na kuwajengea nyumba.

itaendele

Jumanne, 1 Septemba 2015

SAFARI YA ISOKE





Kutokana na naswali la rafiki yangu katalambuga kuwa Nilishindwa kuokota mke ilimradi mke kama vile mtu anavyookota nyanya sokoni na kulipa pesa, nafikiri hata anayeokota nyanya nae huchagua.


Japo kuna usemi usemao mchagua nazi hupata koroma usemi huo niliupinga na kuutupilia mbali.
Niliamini usemi wa kuoa ni kuoa pengine ningefanya hivyo basi ndoa yangu isinge kuwa na
ladha ya unyumba na isingedumu maishani.

Nilijawa na imani kuwa mke mwema hupewa na Mungu, niliishi kwa matumaini ya Mungu na nilitegemea msaada mkubwa kutoka kwake mpaka kipindi hiki Mungu aliwapa Wazazi wangu baraka walikuwa hai wakinisubiri nioe wamuone mkwe na wajukuu wao kabla ya wakat wao wa kufariki kuwa fikia japo Kwa bahati mbaya siku weza kupewa upeo wa kuona mchumba mwema mapema yote hii ambaye angekuwa mke wangu,

japo nilikuwa na kazi nzuri na nafasi yangu kazini ili nifanya nionekane maridadi saa zote.
Watu wengi walio ni ona walinishangaa sana,

itaendelea

Jumatatu, 31 Agosti 2015

SAFARI YA ISOKE

ILIPOISHIA 

Siku Zote nilijibidisha kuwa mfano bora ili niweze kupata mchumba, nilikuwa mtiifu, nikiwa heshimu wenzangu na kushirikiana nao vema kujenga Taifa.Kujaribu kuwa na marafiki wengi wa jinsia tofauti.

ENDELEA 


Nilijitahidi nikihisi pengine wale marafiki wangenifaa kumbahatisha wa ubani wangu.
Pamoja na yote hayo sikuweza kubahatika kupata niliyempenda kutoka moyoni, na aliye ni penda, Nilizidi kumuomba Mungu anishushie neema ya kumpata wa ubani wangu.

Ikafikia wakati nikaomba ushauri, lakini wale niliowaomba ushauri walionekana kuwa fukara wa mawazo, Walinishauri wakisema kuoa ni kuoa.Eti mwanamke ningemfunza mimi mwenyewe kama atakuwa na tabia mbaya.

Nikafikiri mara mia mia ushauri wao nikaona haukuwa na maana zaidi ya upofu.“Bw #kagoma inamaana uwingi wa wanawake ulimwenguni umekosa umpendaye?” Lilikuwa swali nililoulizwa na rafiki yangu katalambuga .Hatahivyo nilishndwa  kumjibu na hatimaye nikamdharau.“Inamaana kuchagua mke wa kuishinae ni kosa????, pengine ni kama kupewa mtihani wa somo usilo jua na kusubiri matokeo mazuri??? au hili swala ni sawa na kuokota fungu la samaki sokoni ama vipi?”Nilijiuliza Maswali mengi bila kujijibu kwa wakati huo.

Itaendelea tena

SAFARI YA ISOKE

Sehemu ya Kwanza


MTUNZI ; Kado¦Kadidi 

                                                   

Nilikuwa nikifanya kazi katika kampuni moja ya usafirishaji wa madini hapa hapa nyumbani Tanzania na wakati fulani nilikuwa natoka njee ya mipaka ya Tanzania kupeleka madini nchi kama  Bang kok nchini Thailand n.k Kampuni yetu ikiwa ya mtu binafsi na ilikuwa wilayani  SIKONGE katika mkoa wa TABORA .

Mimi ni #kagomaKapaku ndiye niliyekuwa idara ya usafirishaji, nikiwa afisa mauzo. Katika maisha yangu yote nilitegemea sana na nilihitaji kuwa na mwenzi wa kuishi naye, kama
vile familia nyingine bora ambazo kila siku zina furaha na ridhaa.Kwa kila mmoja kuwa
mwanandani wa mwenzake. 

Pia nilikuwa namuomba Mungu kwa kila hali si kanisani na hata nikiwa katika mapumziko yangu, anipatie mwanamke ambaye angenifaa katika maisha yangu.Kila siku palipokucha,niliamka nikiwa na wazo la kumpata nimpendaye na anipendaye.Niliamini hivyo japo sikuwa na uhakika kama kweli ningepata mtu kama huyo maishani mwangu.


Siku zote nilijibidisha kuwa mfano bora ili niweze kupata mchumba, nilikuwa mtiifu, nikiwa heshimu wenzangu na kushirikiana nao vema kujenga Taifa.Kujaribu kuwa na marafiki wengi wa jinsia tofauti. Nilijitahidi nikihisi pengine wale marafiki wangenifaa kumbahatisha wa ubani wangu.



itaendelea tena.....